Monday, 23 March 2015

MBIO ZA URAIS NCHINI TANZANIA LOWASA AJITOKEZA HADHARANI, ATANGAZA NIA.

Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa akiwasalimia wanafunzi kutoka vyuo mbalimbali vya mjini Dodoma na waendesha bodaboda walioandamana kwenda nyumbani kwake  kwa ajili ya kumshawishi achukue fomu ya kuwania Urais katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu. 

Siku moja baada ya kuwapokea masheikh 50 kutoka Bagamoyo,  mbunge wa monduli Edward Lowasa  amepokea makundi ya wanafunzi wa vyuo vikuu, madereva wa pikipiki (bodaboda) na wamachinga wa Dodoma wakimtaka achukue fomu kuwania nafasi hiyo.
Tayari mbunge huyo alishampokea Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Dk Rapahel Chegeni na baadaye kundi marafiki wa Lowassa kutoka mikoa ya Tanga, Kilimanjaro na Arusha.
Wanafunzi hao ambao waliongozana na baadhi ya wahadhiri wao walitoka Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom), St John, Mipango na Chuo cha Biashara (CBE), Tawi la Dodoma.

0 comments:

Post a Comment

 

COPYRIGHT © Jicho Duniani DESIGN BY DISMAS TEN 0713216125