![]() |
Askari wa kulinda amani wa umoja wa mataifa wakiwa doria huko Sudan ya kusini ;Darfu |
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limetangaza kwa kauli moja kumuunga mkono Rais wa Yemen, Abed Rabbo Mansour Hadi.
Baraza
hilo pia linaunga mkono suala la kuwepo umoja na mshikamano wa Yemen, huku
kukiwa na onyo kwamba nchi hiyo inaelekea kwenye vita vya wenyewe kwa
wenyewe.
Akizungumza
katika mji wa kusini wa Aden, ambao ameutangaza kuwa mji mkuu wa muda, Rais
Hadi amewataka wanamgambo wa Kishia-Houthi, kuondoka kwenye mji mkuu wa
Sanaa.
Wakati huo
huo, waasi wa Houthi wametangaza upya hatua yao ya kuitwaa miji yote ya
Yemen.
Hatua hiyo
inatokana na mashambulizi ya kujitoa muhanga katika misikiti mjini Sanaa ambapo
watu 137 waliuwawa.
Hapo jana,
waasi wa Houthi waliuteka mji wa Taiz, ambao ni wa tatu kwa ukubwa nchini
Yemen.
0 comments:
Post a Comment