Tuesday, 15 March 2016

POLISI NCHINI TANZANIA IMEWAKAMATA MAKAHABA 287 NA WATEJA WAO KATIKA MSAKO MAALUMU.

0 comments


Jeshi la polisi kanda maalum ya Dar es salaam limefanikiwa kuwakamata jumla ya watu 287 ambao ni dada poa pamoja na kaka poa katika operation maalum iliyofanyika maneo mbalimbali ya Jiji hilo.

Operation hiyo ilitangazwa na kamishna wa kanda maalum mnamo Tarehe 7 mwezi wa 3 na kuazimia kuwakamata madada poa na makaka poa pamoja na wateja wao ambao watakutwa wakiwanunua.

Katika mkoa wa kipolisi wa ilala operation hii imefanikiwa kuwakamata jumla ya madada poa 51 kutoka katika maeneo mbalimbali yakiwemo msimbazi,Buguruni,na stakishari,pia imewakamata jumla ya makaka poa 12 ambapo 11 wanatokea Buguruni na mmoja kutoka msimbazi.

Mkoa wa kipolisi wa temeke umefanikiwa kuwakamata jumla ya madada poa 22,ambapo changombe walipatikana 12,na mbagala walipatikana madada poa 10.

Aidha katika mkoa wa kipolisi wa kinondoni operation hiyo imefanikiwa kuwakamata madada poa 76 kutoka maeneo ya osyterbay madada poa 49,magomeni 23,na kawe madada poa 4,pamoja na makaka poa 4.

Akizungumza na wanahabari jana makao makuu ya polisi kanda maalum ya Dar es salaam ,Kamishna wa kanda hiyo CP Simon Sirro aliwataka watu wenye tabia kama hizo kuacha mara moja kwani ni kinyume na mila na desturi za mtanzania ambapo amewataka kutafuta biashara nyingine halali za kufanya.
SOMA ZAIDI ...

INDIA INAWEZA KUIPA TANZANIA DOLA BILIONI 10 JE NI ZA NN?

0 comments


Tanzania inatafuta msaada wa dola bilioni 10 kutoka kwa wafadhili mbali mbali nchini India kufikia malengo yake ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa miundombinu, hii ni kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa na shirikisho la viwanda nchini India (CII).

Kulingana na ripoti hiyo, fedha hizo zitatolewa na serikali ya India kwa ushirikiano na benki ya Exim ya India pamoja na wawekezaji nchini humo. Aidha ripoti hiyo inasema kuwa shirika linalosimamia makazi nchini Tanzania, National Housing Corporation (NHC) ndilo litakalopokea kiasi kikubwa zaidi cha fedha hizo. NHC itapata dola bilioni 6.2 ikifuatwa na mamlaka ya bandari (Tanzania Ports of Authority) itakayopokea dola milioni 598.


Tanzania pia imetoa ombi la dola bilioni 1.08 kutoka India kufadhili miradi mbali mbali ya ujenzi wa barabara, huku barabara ya Dar es Salaam-Chalinze-Morogoro ikitengewa dola milioni 519. Taifa hilo la Afrika mashariki pia limetoa ombi la dola bilioni 1.3 kufadhili miradi ya nishati na dola milioni 9.1 kufadhili miradi ya kilimo.
SOMA ZAIDI ...

Tuesday, 8 March 2016

BARA LA AFRIKA HUPOTEZA DOLLAR 150 ZA MAREKANI KILA MWAKA KUTOKANA NA RUSHWA.

0 comments
 
 
WAZIRI MKUU wa Tanzania Kassim Majaliwa amesema tatizo la rushwa barani Afrika limesababisha bara hilo lipoteze dola za Marekani bilioni 150 kila mwaka.


Ametoa kauli hiyo leo mchana (Jumanne, Machi 8, 2016) wakati akihutubia wajumbe wa mkutano wa tano wa Bunge la Afrika Mashariki (EALA) linaloendesha vikao vyake jijini Dar es Salaam. Mkutano huo ulioanza Machi 6, utamalizika Machi 18, mwaka huu.


Akizungumza kwa niaba ya Rais Dk. John Pombe Magufuli, Waziri Mkuu alisema rushwa imechangia kwa kiasi kikubwa kurudisha nyuma maendeleo ya Jumuiya hiyo. "Rushwa yaweza kuwa kwa njia kuhonga fedha, kupata fedha kwa kula njama, kujipatia fedha kwa njia za udanganyifu, ama kwa njia za vitisho," alisema.
"Kwa mujibu wa taarifa ya Umoja wa Afrika (AU), rushwa na urasimu vimeainishwa kuwa ni vikwazo vikubwa vinavyochangia kuchelewesha ufanyaji wa biashara kwenye mipaka ya nchi za Jumuiya yetu," alisema.
Amesema sekta binafsi inachukuliwa kama injini ya maendeleo na ukuaji wa uchumi na akatumia fursa hiyo kuipongeza jumuiya ya wafanyabiashara wa Afrika Mashariki kwa kuandaa kanuni za kiutendaji ambazo zimelenga kuhamasisha uadilifu kwenye ufanyaji biashara unaozingatia haki za binadamu, sheria za kazi, utunzaji mazingira na vita dhidi ya rushwa.
 
Akizungumzia kuhusu uondoaji wa vikwazo visivyohusisha kodi (non-tariff barriers) kama njia mojawapo ya kuimarisha biashara kwenye jumuiya hiyo, Waziri Mkuu alisema kwa upande wa Tanzania, vizuizi vya barabarani kwenye barabara kuu ya Kaskazini vimepunguzwa kutoka 50 hadi vitano.


Alivitaja vizuizi vitano vilivyobakia kuwa ni vile vilivyopo kwenye mizni ya Mikese (Morogoro), Nala (Dodoma), Njuki (Singida), Mwendakulima (Shinyanga) na Nyakahura (Kagera).


"Sheria ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya uondoaji wa vikwazo visivyohusisha kodi ilipitishwa Machi 2015 na sasa hivi inaendelea kusainiwa na Wakuu wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki. Pamoja na mambo mengie, nia ya sheria hii ni kuondoa vikwazo vinavyosababisha uagizaji wa bidhaa kutoka nje ya nchi na uuzaji wa bidhaa nje ya nchi, kurahisisha sheria za biashara ndani ya Jumuiya yetu," alisema.


Akizungumzia kuhusu miradi ya uwekezaji ya Jumuiya hiyo, Waziri Mkuu alisema miradi ya ujenzi wa barabara inahitaji kiasi cha dola za marekani bilioni 20; ukarabati na upanuzi wa njia za reli unahitaji dola za marekani bilioni 30; uendeshaji wa mashirika ya ndege na viwanja vya ndege unahitaji dola za marekani bilioni 15; uendelezaji bandari na usafiri wa majini unahitaji dola za marekani bilioni 10; utekelezaji wa miundombinu ya nishati inahitaji dola bilioni 5 ambavyo kwa pamoja vinahitaji dola marekani bilioni 80.


Alisema kuwepo kwa shughuli mbalimbali za kiuchumi ndani ya jumuiya hiyo, kunaifanya Jumuiya ya Afrika Mashariki kuhesabika kuwa ni jumuiya yenye nguvu kubwa ya kiuchumi barani Afrika.
SOMA ZAIDI ...

Monday, 7 March 2016

KOREA KASKAZINI KUIPIGA MAREKANI KWA BOMU LA NYUKLIA MUDA WOWOTE NI HATARI HII.

0 comments





Korea Kaskazini imetishia kutekeleza mashambulio ya nyuklia dhidi ya Korea Kusini na Marekani iwapo nchi hizo mbili zitaendelea na mazoezi ya pamoja ya kijeshi.

Mazoezi hayo, ambayo hufanyika kila mwaka, mwaka huu yatashirikisha wanajeshi 300,000.

Serikali ya Korea Kaskazini imetoa taarifa ya ikitishia kutekeleza “shambulio la nyuklia kwa ajili ya haki”.

Ni kawaida kwa Pyongyang kutoa vitisho vya aina hiyo na wataalamu wanatilia shaka uwezo wa Korea Kaskazini kuwa na makombora ya nyuklia.

Hisia hupanda kati ya Korea Kaskazini na Korea Kusini na Marekani kila mazoezi hayo ya pamoja ya kijeshi yanapofanyika.

Pyongyang hutazama mazoezi hayo kama mazoezi ya kujiandaa kuivamia.

Mwaka uliopita, Korea Kaskazini ilitishia kugeuza Washington kuwa “bahari ya moto”.

Wizara ya ulinzi ya Korea Kusini imeionya Pyongyang dhidi ya “hatua za haraka zisizo za busara ambazo zinaweza zikailetea maangamizi”.

Mazoezi ya mwaka huu, yanayoshirikisha wanajeshi 300,000 wa Korea Kusini na 15,000 wa Marekani, ndiyo makubwa zaidi kuwahi kufanyika.

Yanaandaliwa siku chache tu baada ya Umoja wa Mataifa kuidhinisha vikwazo vipya dhidi ya Korea Kaskazini kutokana na hatua yake ya kufanyia majaribio bomu la nyuklia na kufyatua makombora.

Korea Kaskazini ilijibu vikwazo hivyo kwa kutangaza itaweka tayari silaha zake za nyuklia na pia ikavyatua makombora ya masafa mafupi baharini.
SOMA ZAIDI ...

Thursday, 3 March 2016

NI HUZUNI NA HURUMA MIZOGA 34 YA VIFARU YAPATIKANA.

0 comments


Ni uzuni kusikia yakwamba polisi nchini Namibia wamepata mizoga 34 za vifaru katika operesheni ya angani katika kipindi cha miezi miwili iliyopita mwaka huu.

Ishirini na tisa ya mizoga zilipatikana katika mbuga la wanyama pori la Etosha ambayo ina idadi kubwa ya vifaru nchini.

Mizoga tano zilipatikana katika shamba binafsi. Vipimo vya DNA zinaendelea ili kubaini kama vifaru waliuawa.
SOMA ZAIDI ...

Wednesday, 2 March 2016

BAADA YA SUDANI YA KUSINI KUJIUNGA NA UMOJA WA AFRIKA MASHARIKI SOMALIA KUFUATA?

0 comments


Nchi ya Sudan kusini imekuwa ya sita kuwa na uanachama na Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC),baada ya mkutano wa kilele wa Wakuu wa kanda wa Jimbo kukaribisha nchi ile ndogo kujiunga na EAC.

Mwenyekiti wa mkutano wa Wakuu wa EAC na Rais wa Tanzania John Magufuli alitangaza haya katika ufunguzi rasmi wa mkutano huo uliofanyika mjini Arusha, kaskazini mwa Tanzania.

Mkutano huo wa mkoa ulihudhuriwa na Rais wa Uganda Yoweri Kaguta Museven,Rais wa Rwanda Paul Kagame,Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta na Rais wa Tanzania John Magufuli,huku nchi ya Burundi ikiwakilishwa na Makamu wa Rais wake.


Magufuli alisema kuwa kujiunga na EAC italeta faida nyingi kwa watu wa Sudan kusini.
SOMA ZAIDI ...

DR SLAA AFUNGA NDOA KWA MBWEMBWE TAZAMA PICHA.

0 comments


Hatimaye aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Wilbroad Slaa amekamilisha ndoto yake kubwa baada ya jana kufunga ndoa na mpenzi wake, Josephine Mushumbusi nchini Canada. Ingawa Dk. Slaa aliwahi kuwa Padri wa Kanisa Katoliki, wawili hao wanadaiwa kufunga ndoa kwenye kanisa tofauti la Kikristo ingawa jina la kanisa hilo halikufahamika mara moja. Jaribio la kufunga ndoa kwa wawili hao tangu mwaka 2010 lilikumbwa na vizingiti ikiwa ni pamoja na mume wa zamani wa Josephine kufungua kesi mahakamani akidai kuwa bado mwanamke huyo ni mkewe halali.
SOMA ZAIDI ...
 

COPYRIGHT © Jicho Duniani DESIGN BY DISMAS TEN 0713216125